Thursday, November 16, 2017

Zimbabwe bado hali ni tata baada ya jeahi kuchukua nchi

Watu nchini Zimbabwe wanasubiri kuona hatua ambazo jeshi litachukua baada ya kutwaa madaraka ya nchi hiyo.

Rais Robert Mugabe yuko katika kizuizi cha nyumbani mjini Harare lakini ripoti ambazo hazijathibitishwa zinasema kuwa mke wake Grace ambaye alikuwa anataka kumrithi akimekimbia kwenda Namibia

Hatua za kijeshi zilifuatia kufutwa kwa Makamu wa Rais Emmerson Mnangagwa ambayr ni hasimu mkubwa wa Bi Grace Mugabe.

Mahala alipo Mnangagwa pia hapajulikani.

Lakini mzozo kuhusu ni nani anaweza kumrithi Mugabe kati ya Bi Grace Mugabe na Bwa Mnangagwa umekigawanya chama cha Zanu-PF miezi ya hivi karibuni.

Share This
Previous Post
Next Post

Ajiraperfect provides a full online service for anyone looking for a new jobs everyday. We're not a recruitment agency,insteady it is JOB SITE.We advertise Latest job vacancies on behalf of employers and recruitment agencies who are looking for Employee

0 coment�rios: