Watu nchini Zimbabwe wanasubiri kuona hatua ambazo jeshi litachukua baada ya kutwaa madaraka ya nchi hiyo.
Rais Robert Mugabe yuko katika kizuizi cha nyumbani mjini Harare lakini ripoti ambazo hazijathibitishwa zinasema kuwa mke wake Grace ambaye alikuwa anataka kumrithi akimekimbia kwenda Namibia
Hatua za kijeshi zilifuatia kufutwa kwa Makamu wa Rais Emmerson Mnangagwa ambayr ni hasimu mkubwa wa Bi Grace Mugabe.
Mahala alipo Mnangagwa pia hapajulikani.
Lakini mzozo kuhusu ni nani anaweza kumrithi Mugabe kati ya Bi Grace Mugabe na Bwa Mnangagwa umekigawanya chama cha Zanu-PF miezi ya hivi karibuni.
0 coment�rios: